This version of the page http://www.voaswahili.com/a/china/3373341.html (0.0.0.0) stored by archive.org.ua. It represents a snapshot of the page as of 2016-06-22. The original page over time could change.
Shambulizi kwenye uwanja wa ndege China lajeruhi watu 4

Upatikanaji viungo

  • Nenda habari kuu
  • Nenda katika urambazaji
  • Nenda katika tafuta
Lugha
Habari

Shambulizi kwenye uwanja wa ndege China lajeruhi watu 4


Walinzi katika uwanja wa ndege wa Pudong Shanghai, China

  • Shirikiana kwenye Facebook
  • Shirikiana kwenye Twitter
  • Mpelekee rafiki kwa barua pepe

Maafisa nchini China wanasema,mwanamme mmoja aliyekuwa na milipuko iliyotengenezwa nyumbani, alijeruhi watu 3 katika eneo la ukaguzi la uwanja wa ndege wa Shanghai, katika juhudi za kujiuwa mwenyewe.

Mwanamume huyo ambaye hajatambuliwa aliondowa chupa zilokuwa na vifaa vya kulipuka kutoka kwenye mkoba wake kabla ya kurusha chupa moja katika eneo la Terminal Two kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Pudong mjini Shanghai, maafisa wanasema.

Mwanamume huyo alitowa kisu, na kujikata shingo. Maafisa wanasema kuwa mwanamume huyo sasa yuko katika hali mahtuti hospitalini.

Lengo lake halikuwa bayana.

Waathirika wanne walijeruhiwa a vipande vya vigae na wanatibiwa hospitalini, hayo ni kwa mujib wa shirika la habari la China Xinhua.

Tukio hilo lilivuruga shughuli kwenye eneo la ukaguzi kwenye uwanja wa ndege, lakini baadae hali ilirejea kuwa ya kawaida.

Uwanja wa ndege ulikuwa umejaa watu waliokuwa wanarejea nyumbani baada ya siku ya mapumziko, siku chache tu kabla ya kufunguliwa kwa uwanja wa michezo Wa Disley hapo alhamisi mjini Shanghai.

Huenda ukapenda pia

  • Habari

    Mshambulizi ya Boko Haram yapelekea ukosefu wa usalama wa chakula kukithiri Diffa, Niger.

  • Kenya

    Jumba la maonyesho la Smithsonian Marekani, kufanya onyesho la kwanza kuu la Quran

  • VOA60 Afrika

    VOA60 Africa: Mashirika ya kutowa misaada yahangaika kugawa maji kwa wakimbizi waliopo jangwani

  • Video

    Mahojiano wa VOA na katibu mkuu wa CUF Seif Shariff Hamad

  • Habari

    Jean-Piere Bemba ahukumiwa miaka 18 jela

Back to top
XS
SM
MD
LG