This version of the page http://www.voaswahili.com/a/3372595.html (0.0.0.0) stored by archive.org.ua. It represents a snapshot of the page as of 2016-06-22. The original page over time could change.
Watu 50 wauwawa katika klabu Orlando, Marekani

Upatikanaji viungo

  • Nenda habari kuu
  • Nenda katika urambazaji
  • Nenda katika tafuta
Lugha
Marekani

Watu 50 wauwawa katika klabu Orlando, Marekani


Meya wa Orlando Buddy Dyer, katikati, na mkuu wa polisi wa Orlando John Mina, kushoto, wawasili kuzungumza na waandishi habari kuhusu shambulizi la klabu ya Pulse Orlando Orlando, Fla., June 12, 2016.

  • Shirikiana kwenye Facebook
  • Shirikiana kwenye Twitter
  • Mpelekee rafiki kwa barua pepe

Mshambulizi mwenye asili ya Afghanistan amewauwa karibu watu 50 katika klabu moja ya usiku mjini Orlando, katika jimbo la Florida nchini Marekani, na kuwajeruhi zaidi ya wengine 50 kabla ya polisi kuvamia klabu hiyo na kuwaokoa walonusurika.

Afisa mmoja wa polisi aliyekua anafanyakazi kama mlinzi katika klabu hiyo ya Pulse, anasema alianza kufyetuliana risasi na mshambulizi karibu saa nane usiku, kabla ya mshambulizi kuwachukua mateka baadhi ya wateja wa klabu hiyo.

Maafisa wa usalama wakizungumza na waandishi habari Jumapili asubuhi wanamtaja mshambulizi kua ni Omar Saddiqui Mateen, ambae wazazi wake wanaotokea Afghanistan, na yeye alizaliwa Marekani.

Maafisa wa idara ya upelelezi wa masuala ya jinai hapa Marekani FBI, wanafanya uchunguzi na kulichukulia shambulizi hilo kama la kigaidi kwa wakati huu lakini hawana uhakika sababu za kushambuliwa kwa klabu hiyo inayowahudumia zaidi wapenzi wa jinsia moja.

Maafisa wanasema shambulizi hilo ndilo baya kabisa la mauwaji ya bunduki ya haliaki kutokea Marekani.

Mkuu wa Jamii ya Waislamu huko Florida ya kati Muhammad Musri amelaani kitendo hicho na kutoa wito kwa watu wote kuungana na kuwaombea waathiriwa, na kuomba kukomeshwa kwa mashambulizi ya halaiki yanayofanyika Marekani.

Shambulio hilo linafuatia jingine lillotokea katika mji huo siku moja kabla, pale muimbaji Christine Grimmie, kijana mwenye umri wa miaka 22, mashuhuri kwenye YouTube, alipouliwa alipokua anawapokea mashabiki wake baada ya kuimba.

Muimbaji wa The Voice Christina Grimmie

.

Huenda ukapenda pia

  • Alfajiri

    Alfajiri

  • Jioni

    Jioni

  • VOA Express

    VOA Express

  • Alfajiri

    Alfajiri

  • Jioni

    Jioni

  • VOA Express

    VOA Express

  • Alfajiri

    Alfajiri

  • Jioni

    Jioni

  • Jioni

    Jioni

  • Jioni

    Jioni

Facebook Forum

Back to top
XS
SM
MD
LG