This version of the page http://www.voaswahili.com/a/3539214.html (0.0.0.0) stored by archive.org.ua. It represents a snapshot of the page as of 2016-10-16. The original page over time could change.
Al-Shabab yaua watu sita Mandera, Kenya

Upatikanaji viungo

  • Nenda habari kuu
  • Nenda katika urambazaji
  • Nenda katika tafuta
Lugha
Habari

Al-Shabab yaua watu sita Mandera, Kenya


Map of Mandera, Kenya

  • Shirikiana kwenye Facebook
  • Shirikiana kwenye Twitter
  • Mpelekee rafiki kwa barua pepe

Gavana wa jimbo la Mandera nchini Kenya, Ali Roba, amethibitisha kuwa watu sita wameuawa na mmoja kupata majeraha mabaya baada ya watu waliokuwa wamejihami na wanaoaminika kuwa wanachama wa kundi la Al-Shabaab, kushambulia jingo la makazi katika mji wa Mandera karibu na mpaka wa Kenya na Somalia.

Kwa mujibu wa ujumbe aliouandika katika ukurasa wa Twitter, Roba alielezea masikitikao yake na kuzifariji familia za waliopoteza maisha yao. ”Vifo sita ni vingi mno," alisema kwenye ujumbe huo.

Gavana huyo alisema kuwa maafisa wa usalama walijibu shambulio hilo na kuweza kuwaokoa watu 27, ikiwa ni pamoja na mtu aliyejeruhiwa, kutoka jingo hilo.

Mkazi mmoja wa mji wa Mandera amesema kuwa nyumba iliyoshambuliwa inamilikiwa na wizara ya wafanyakazi ya Kenya na kwamba wengi waliokuwemo ni wafanyakazi wa serikali na wanakandarasi waliokuwa wanajenga ua lililozua utata, kwenye mpaka.

Huenda ukapenda pia

  • Habari

    Mrepublican Donald Trump asema uchaguzi Marekani umeibwa

  • Washington Bureau

    Trump akabiliwa na utata zaidi katika kampain zake

  • Habari

    Kampeni za uchaguzi Marekani zachukua mrengo mwingine

  • Afrika

    Tume ya uchaguzi Ghana yazuiya wagombea kushiriki uchaguzi

  • Marekani

    Galaxy Note 7 yapigwa marufuku ndani ya ndege

Facebook Forum

Back to top
XS
SM
MD
LG